Pages

Subscribe:

Ads 468x60px

Wednesday 13 January 2010

TETEMEKO LA ARDHI LAIKUMBA HAITI!!


Maelfu wanahofiwa kufa kufuatia tetemeko hilo lililotokea nchini Haiti ambalo lilikuwa la kipimo cha 7.3 katika vipimo vya Ritcher.
Ripoti zinasema uharibifu mkubwa umetokea katikati mwa mji mkuu wa Port-au-Prince. Baadhi ya majengo yaliyoharibiwa vibaya ni ikulu ya rais na hospitali moja mjini humo.

Msemaji wa umoja wa mataifa mjini New York Martin Nesirkyo amethibitisha kuwa ofisi za umoja wa mataifa mjini Port-au-Prince zimeharibiwa. Amesema pia kuwa idadi kubwa ya watu wamezikwa chini ya vifusi na wengine kufa au kujeruhiwa.

Waziri wa mambo ya nje wa Marekani Hilary Clinton amesema Marekani tayari imeanza kutuma misaada ya dharura.

0 comments: