Pages

Subscribe:

Ads 468x60px

Friday 28 February 2014

TASWIRA KUTOKA SOKO KUU LA SANYA JUU MKOANI KILIMANJARO

Sanya Juu ni mji mdogo ndani ya wilaya Siha Mkoani Kilimanjaro ikiwa ni Km 25 toka Bomang'ombe  na KM 50 toka Moshi Mjini, weekend hii nilifanikiwa kuutembelea Mji wa Sanya Juu ambapo siku ya Jumamosi  mji huu huwa umechangamka kwa shamrashamra za kibiashara. katika pita pita zangu nilifanikiwa kulitembelea soko ila nilishangazwa na hali niliyo ikuta ya miundombinu isiyo kidhi na kulifanya soko kuonekana hatarishi kwawafanya biashara na wateja wao kiafya.
Huu ni msimu wa mvua kwa sehemu kubwa ya mkoa wa Kilimanjaro, hatua za haraka zinatakiwa kuchukuliwa kuimarisha miundombinu ya soko la Sanya Juu kuimarisha afya za wafanyabiashara na wateja wao. 

Hii ni njia ya kuelekea soko hili ikiwa imejaa matope kutokana na kuwa katika kiwango cha changarawe

Baadhi ya wachuuzi wakiwa sokoni hapo kununua mahitaji yao lakini mazingira ya soko hayaridhishi kutokana na uchafu uliokithiri hapo na kuhatatrisha afya za walaji wa bidhaa

hali halisi inavyonekana sokoni hapo baada ya mvua kunyesha

Msimu huu wa mvua unasababisha kero hii kwa baadhi ya wateja hata wafanyabiashara sokoni 

hali hii pia ni kero kwa watembea kwa miguuu  sokoni hapo 

Picha zote na mdau Wito Msafiri wa Mwanaharakati Mzalendo Blog

1 comments:

Yasinta Ngonyani said...

Kila la kheri kwa shughuli.