Pages

Subscribe:

Ads 468x60px

Saturday 21 August 2010

MKULIMA BORA WA MWAKA!

ulikuja upepo wa ajabu ukaziangusha nyanya,...nikaziinua na kuzifunga kamba kwa unyonge huku nikiwa nimekata tamaa ya kuuendelea kukua.
What a best mkulima, ona manyanya yanavyopendeza hahahaaa

Furaha ya mkulima siku zote ni kuvuna kile alichopanda,nami leo nina furaha ya ajabu kuvuna mazao yangu (nyanya) sikutegemea kama zingekuwa hivi...i mean zina afya, zinapendeza na ziko tayari kuvumwa.Sina budi kujiita mkulima bora wa mwaka.

6 comments:

Yasinta Ngonyani said...

Ni kweli wewe mkulima bora wa mwaka. Ila usinisahau mimi na mboga zangu labda tubadilishana nipe nyanya nikupe mboga za majani(maboga nyamuza) Naona sasa Coop extra na ICA hawatakuona tena. Hongera Edna.

Bennet said...

Hongera sana ila pia shukuru kwamba hazikushambuliwa na magonjwa maana ingebidi uonane na wataalam wakushauri zaidi

PASSION4FASHION.TZ said...

Mnyalukolo kamwene?hahahahahaaaaa! wewe kweli mkulima bora wa mwaka,mkulima wewe kweli nyanya zimestawi, ila mashaka kidogo hapo shamba lako lina ukubwa gani?...kwi kwi kwi, umekumbuka za Ilula nini....kazi nzuri mtani wangu kaza buti.

EDNA said...

Yasinta kina: COOP na ICA bye bye.
Bennet: asante wadudu hawakushambila nyanya,
Passin4fashion:(Mtani),sisi wanyalukolo kwa kulima ndio zetu....Ukubwa wa shamba nitakuambia nikimaliza kuvuna.

emu-three said...

Hongera kwa kulima bora wa mwaka, na uzuri wa nyanya ni kachumbari! Na vyema dada Yasinta kasema mgeane nyanya kwa mboga, na uzuri wa mboga ni kuungwa kwa nyanya, kweli nyie ni wakulima wa mwaka.
Kwani licha ya upepo, wadudu na viangamizi vingine mumeweza kuzistawisha vitamini, mpenzi wamwili! Nashukuru kwa hilo.
Wakati nyie mnajipa `umwaka' wengine wapo mauaakwani wakiutafuta `uanasiasa wa miaka mitano'....
Jukwaani kuna vikwazo, kuna upepo mkali unaweza ukamuangusha mtu..halafu utasikia..eheeee, kalogwa eeehe, hili na lile!
Bora yako mwenzetu ulichukua kamba ukazifunga nyanya zako na huyo unajivunia, labda na hawo wanaotafuta kura zao watajua siri hiyo, ili mwisho wa siku tupate mwanasiasa wa

EDNA said...

Haahaa Emu three umeniacha hoi na mashairi yako.