Pages

Subscribe:

Ads 468x60px

Saturday 18 September 2010

VIPI TENA DADA?



Mwanamuziki wa kizazi kipya nchini ambaye alikuwa Mwanachama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) mkoani Arusha, Nakaaya Sumari, ametangaza kukihama chama hicho na kujiunga na Chama Cha Mapinduzi (CCM). Nakaaya katangaza hayo mbele ya mgombea urais wa CCM Jakaya Kikwete katika Uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha wakati wa mkutano wa kampeni za Wilaya ya Arumeru.

5 comments:

Yasinta Ngonyani said...

Labda amestuka yaani machale yake yamemwambia CCM itashinda...ni wazo tu!!

o'Wambura Ng'wanambiti! said...

ngoja aende huko labda atakuwa mbunge wa kututea au akawe Miss Politian!

EDNA said...

Yasinta labda kweli machale yamemcheza:
Chacha umeniacha hoi akawe miss Politician?

ADELA KAVISHE said...

mmmh mbona wengi wanahama nyakati za majeruhi...

Anonymous said...

Achahama Chadema kaingia January akinusa kupata viti maalum kakukuta makamanda wanamabinduzi hakuna rushwa rushwa kakosa hata ujumbe wa nyumba kumi kakimbilia CCM kula matapishi yake maana alitukana sana, CCM wasivyo na hila wakampokea akale matapishi yake aliyoimba kwenye Mr Politician