Pages

Subscribe:

Ads 468x60px

Friday 20 May 2011

SHILINGI MIA MOJA KUSAFISHWA MIGUU.

Waswahili wanasema mjini shule,.kila kitu na kila hali yaweza kuzalisha fedha ikiwa tu wateja watapatikana
.Ni akili yako tu.Kijana akiwajibika kumsafisha miguu mteja katika soko la Tandale, gharama yake ni shilingi mia moja (100) kwa miguu yote miwili.
HALALI MTU NJAA HAPA.
Photo credit to Wavuti.

3 comments:

Yasinta Ngonyani said...

Haki ya nane kujituma ndio kipato usimwone mjinga kesho na kesho kutwa atajenga nyumba na wewe unayeoshwa huna hata pa kujificha mvua...

emu-three said...

Kazi ni kazi bora kitu kiingie kinywani...au sio mjini shule!

Goodman Manyanya Phiri said...

Haya basi, kazi kwao wanasiasa wanaodai wao ni wenye nia ya kunyanyua uchumi wa Afrika. Vijana kama huyo!!! Na hakuna mfano kumpita kwa wale wanaostahili kusaidiwa na serikali ili waendeleze biashara zao.

Yeye sie mwoga kuwaza na kutekeleza mawazo yake. Kibiashara anamoyo wasimba kwani anakitu Wazungu huita ENTREPRENEURIAL SPIRIT!