Pages

Subscribe:

Ads 468x60px

Thursday 23 December 2010

Obama asaini sheria ya mashoga jeshini



Rais Barack Obama ametia saini sheria ambayo kwa mara ya kwanza itaruhusu mashoga jeshini kuwa wazi na hali zao za kijinsia bila ya kuwa na wasiwasi wa kufukuzwa kazi.


Rais Barack Obama
Rais Obama amesema mabadiliko hayo yataimarisha jeshi na kwamba ilikuwa ni hatua sahihi ya kuchukua.

Katika sera ya zamani, iliyojulikana kama "Usiulize, Usiseme" iliruhusu mashoga kufanya kazi jeshini, lakini kwa kuweka hali ya jinsia zao siri.

Sera hiyo ilianzishwa miaka kumi na saba iliyopita wakati wa utawala wa rais Bill Clinton, ikichukua nafasi ya kupiga marufuku mashoga jeshini.
Chanzo BBC

3 comments:

Simon Kitururu said...

Kuna mambo mengine nafikiri ni matatizo ya nchi zilizoendelea ukizingatia Tanzania bado hata uhakika wa mlo tukiachilia mbali yale ya LAKSHARI kama ya UMEME viongozi wetu wanashindwa kuyashughulikia!


Na tukumbuke kuwa labda kwakuwa KISWAHILI ndio baadhi ya lugha chache ziwezazo mpaka kuainisha mpaka aina ya usenge kwa kutambua kuna BASHA na MSENGE- basi labda inamaana labda haya mambo yako tu kwa wingi katika jamii izungumzayo kiswahili na tamaduni ingeruhusu ungeweza kukuta tunawanajeshi na VIONGOZI lukuki ambao kama sio mabasha basi ni WASENGE -tukiachilia mbali WASAGAJI - kwa vitendo vyao vya kushughulikia wenzao wenye jinsia kama yao kiasherati.

Anonymous said...

Duh! kama Bongo ingepitishwa sheria hii wazi huenda tungeona baadhi ya viongozi ni mashoga.

Yasinta Ngonyani said...

Watu weweeeeeeee! sisemi sana.